Daily Poll
Our services improving?
Visitors
SHEREHE ZA KUADHIMISHA MIAKA KUMI YA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umeadhimisha miaka kumi kwa kutoa tuzo kwa mashujaa mbalimbali waliochangia katika mafanikio yake tangu kuanzishwa. Mashujaa hao ni pamoja na viongozi wakuu wa serikali wastaafu, mawaziri wastaafu, viongozi wa vyama vya wafanyakazi, watumishi wa serikali wastaafu na waandishi wa habari.
WAFANYAKAZI WA NHIF WAASWA KUTOBWETEKA NA MAFANIKIO

NHIF MSHINDI WA JUMLA KWA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII AFRIKA

Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Emanuel Humba (anayeongea) ikiwa pamoja na maafisa wengine waandamizi wa NHIF akiongea na waandishi wa habari kuhusu tuzo ambazo NHIF imetunukiwa baada ya kuibuka mshindi wa jumla kwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii barani Afrika. Tuzo hizo zilitolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (ISSA) katika mkutano iliyofanyika Mjini Arusha kati ya tarehe 5-6 Desemba 2011 ambapo Raisi wa ISSA Bw. Errol Frank Stoove alikabidhi tuzo hizo.















