Daily Poll
Our services improving?
Visitors
NHIF MSHINDI WA JUMLA KWA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII AFRIKA

Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Emanuel Humba (anayeongea) ikiwa pamoja na maafisa wengine waandamizi wa NHIF akiongea na waandishi wa habari kuhusu tuzo ambazo NHIF imetunukiwa baada ya kuibuka mshindi wa jumla kwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii barani Afrika. Tuzo hizo zilitolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (ISSA) katika mkutano iliyofanyika Mjini Arusha kati ya tarehe 5-6 Desemba 2011 ambapo Raisi wa ISSA Bw. Errol Frank Stoove alikabidhi tuzo hizo.
UZINDUZI WA KAMPENI YA ELIMU YA WAZI YA VIELELEZO

Mfuko wa Taifa wa Bima ya NHIF hivi karibuni umezindua Kampeni ya Elimu ya Wazi ya Vielelezo kwa Umma. Kampeni hiyo iliyozinduliwa mjini Bagamoyo inalenga kuwapelekea elimu wananchi kuhusu shughuli za Mfukowa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kwa kutumia gari la matangazo na sinema.
WANAOSAINISHA WANACHAMA NHIF KABLA YA HUDUMA KUKIONA
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kanda ya Moshi, umewaonya Watoa huduma wanaowalazimisha wanachama wake kuweka saini katika fomu za matibabu kuwa wamewatibu wakati hawajafanya hivyo na kuahidi kuchukua hatua kali za kisheria dhidi yao.















