Mafao Yatolewayo

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ulianzishwa ili kusimamia upatikanaji wa huduma za matibabu kwa watumishi wa Serikali, Umma, Binafsi, Wanafunzi na makundi mbalimbali ya watu ili kupata huduma za matibabu kupitia vituo vya kutolea huduma za afya vyaSerikali, Madhehebu ya dini, Binafsi na Maduka ya Dawa ambayo yamesajiliwa na Mfuko ndani na nje ya nchi.

WALENGWA WA HUDUMA ZA NHIF

  • Watumishi wa Taasisi za Umma na Serikali,
  • Watumishi wa Sekta binafsi za ajira,
  • Watumishi wa Madhehebu ya dini
  • Madiwani
  • Wanafunzi wa Shule, Taasisi za Elimu na Vyuo vya Elimu ya Juu
  • Watu binafsi
  • Watoto chini ya miaka 18

KWANINI UCHAGUE NHIF?

  • Ina mtandao mpana wa vituo vya matibabu zaidi ya9,194 nchi nzima.
  • Inagharamia matibabu sawasawa kwa wanachama wakekadri ya vitita vya mafao vya kila mwanachama.
  • Huduma za matibabu hutolewa kadri ya mahitaji na ushauri wa daktari.
  • Mwanachama ana nafasi ya kusajili wategemezi wake kulingana na taratibu zilizopo.
  • Kadi ya NHIF hutumiwa katika kituo chochote cha afya kilichosajiliwa na NHIF popote Tanzania bara na Zanzibar.
  • Mwanachama mstaafu wa sekta ya umma ana nafasi ya kuendelea kutibiwa na NHIF bila kuendelea kuchangia kwa kufuata taratibu zilizowekwa.

KITITA CHA MAFAO

Kwa kuzingatia mahitaji halisi ya kimatibabu, hivi sasa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya unalipia huduma zote za kimatibabu kwa wanachama wake.

Mfuko wa Bima ya Afya unatoa mafao yafuatayo kwa wanachama wake:

1. Kujiandikisha na Ushauri wa daktari.

2. Vipimo zaidi ya 350 vya msingi na maalum kama CT-Scan na MRI.

3. Dawazilizosajiliwa na zinazoruhusiwa kutumika hapa nchini.

4. Huduma za kulazwa kwa daraja la kwanza au la pili kulingana na makubaliano kati ya Mfuko na Watoa huduma.

5. Upasuaji mdogo, mkubwa, bingwa na kibingwa Bobezi.

6.Huduma za afya yakinywa na meno

7. Matibabu ya macho na uoni.

8.Huduma za mazoezi ya viungo (physiotherapy and rehabilitation)

9.Miwani ya kusomea kwa mwanachama mchangiaji

10. Matibabu kwa Wastaafu na wenzi wao

11. Vifaa saidizi (Medical/ Orthopedic appliances) kama Fimbo nyeupe, magongo, vifaa vya usikivu, vifaa shikizi vya shingo, n.k.

HUDUMA ZINAZOHITAJI VIBALI MAALUM

Ili kupata huduma za matibabu zinazohitaji vibali maalumu mwanachama hatalazimika kwendaofisi ya mkoa kufuata kibali kama hapo awali. Vibalivinaombwa na mtoa huduma katika mfumo na Mfuko hutoa idhini ya vibali katika Mfumo na mwanachama huendelea kupatiwa huduma hizo.

Huduma hizi ni pamoja na:-

  • 1.Kipimo cha MRI na CT-Scan
  • 2.Vifaa tiba saidizi (Orthopaedic Appliances)
  • 3.Huduma ya nyenzo saidizi (Implants)
  • 4.Huduma za miwani ya kusomea kwa mwanachama mchangiaji.

Mwanachama anayehitaji kupata baadhi ya huduma za vibali maalum kwa mara ya kwanza atafunguliwa faili katika ofisi iliyo karibu nae. Atakapohitaji kibali hicho hicho kwa mara ya pili atahudumiwa huko huko hospitali.

Huduma hizi ni pamoja na:

  • 5.Huduma zakuchuja damu (Haemodialysis)
  • 6.Dawa za kuongeza uzalishaji wa damu (Erytrhropoietin)
  • 7.Dawa za Saratani (Chemotherapy)
  • 8.Huduma kwa waliopandikizwa Figo (Immuno-suppressants/ Immuno-stimulants)
  • 9.Huduma za tiba yamionzi (Radiation Therapy)
  • 10.Huduma za upasuaji wa Moyo (Advanced Cardiac surgical Services)